Website za Wapendwa


Thursday, October 13, 2011

Jitambue Ya Chris Mauki.....SABABU MBOVU ZA KUINGIA KATIKA NDOA

Watu wengi tumewaona kwenye ndoa wakiishi katika hali tofauti za maisha, wako wenye fedha na wasionazo, wako wenye furaha na wasio na wasionao. Yote hii huweza kuchangiwa na sababu nyingi ikiwemo wanandoa hawa kujikuta wanaingia katika ndoa wakisukumwa na sababu zilizo mbovu na zisizo na msingi. 

Ziko sababu njema na nzuri za ndoa zinazoongelewa sana na wengi maeneo mbalimbali.  Mimi nimejaribu kuzitafuta zile sababu zisizo nzuri ambazo wengine pasipokuwa makini wamezishikilia na kusiruhusu sababu hizi ziwasindikize katika ndoa na hivyo kujikuta wenajuta na kulia katika muda mwingi wa maisha.

Hii pia ni sababu ya ukweli kwamba siku hizi idadi ya ndoa zinazovunjika ni kubwa sana kuliko zamani.  Hali ya kiwango cha kudhamiria (commitment) kwa wanandoa ni kidogo sana na hivyo kushusha uthamani wa ndoa zenyewe.
Sababu hizi zitakuwezesha kuubadili mtazamo ulionao juu ya ndoa na kukupelekea kubadili namna  unavyo sema au kuwaza au kutenda kuhusiana na suala zima la ndoa.

SABABU MBOVU
  1. Kuingia katika ndoa kwa lengo la kusaidiwa au kuongeza  kiwango cha kiuchumi ulicho nacho.  
hapa wengine wamewageuza wapenzi wao kuwa mitaji au rasilimali ya kuwaondoa wao pamoja na ndugu zao kutoka kwenye umasikini.  Kwa kuthibitisha hili wengine  wamepewa majina kama BUZI, ATM n.k.

Katika penzi la namna hii hakuna mguso au muunganiko wa kuhisia baina ya wapenzi, bali kinachowaunganisha pekee ni kile kilicho mfukoni. Athari za penzi la aina hii lina fungua milango mingi kwa wanandoa  kutokuwa  waaminifu na hata kujihusisha na mapenzi  nje ya ndoa.

  1. Hofu ya umri kupita na kuzeeka
Wako wengi sana, hususani watu wa wajinsia ya kike ambao wamejikuta wakiwakubali wanaume wa aina yoyote ili mradi tu nao waolewe maana umri wao ulionekana kusonga sana na hofu ya kutoolewa kutanda.
Mwanaume anayehusiana na mwanamke mwenye tabia hii huulizwa au kulazimishwa kila siku kwenda kujitambulisha kwa wazazi wa binti au kutangaza ndoa.  Ndoa nyingi za aina hii zimeishia kenye talaka na kutengana.
Wako wengine ambao, kwasababu wanakiu sana ya kupata watoto na wameogopeshwa sana habari kwamba wana weza wasipate watoto kwa sababu ya umri wao, basi watacheka  na kaka yeyote yule ilimradi tu waolewe au wazae naye  Wengine wajinsi hii wamejuta sana baada ya kujikuta kuwa waliyezaa naye hakuwa BABA wa kweli bali kirukanjia tu na kwahiyo wameishia kulea mtoto au watoto wao wenyewe pasipo mzazi wa pili, jambo ambalo kwa kiasi kikubwa  linawaathiri watoto wengi.  Kwa wale wanaokimbilia kuolewa ili wakazae watoto, kukumbuka kuwa hata huko kwenye ndoa kuna waliokosa watoto.

  1. Kuingia kwenye ndoa sababu ya mimba au mtoto aliyepatikana kabla ndoa
Lazima kutofautisha kuwa sababu iliyowapelekea kuzaa mtoto siyo itakayowapelekea kuoana.  Acha sababu ya kuoana kwenu iwe penzi lenu la dhati na sio mimba au mtoto.

Suala hili linahitaji pia wazazi wajue kwamba kitendo cha watoto  kupeana mimba au kupata mtoto hakitoshi kuwa sababu ya kuwalazimisha kuoana, maranyingi wazazi wamewalazimisha watoto wao kuingia katika ndoa sababu ya mimba au mtoto na kujikuta wanawaharibia maisha yao mazima.  

  1. Kulazimika kuingia kwenye ndoa au mahusiano ya kudumu kwasababu ya upweke, (Loneliness). Mara nyingi mtu anapokuwa peke yake (single) huwaza kuwa ndoa ndiyo inayoweza kuwa utatuzi mkubwa wa matatizo yake.  Nakubaliana na ukweli wa maandiko kwamba “Sio vema mtu awe peke yake…” lakini ni vizuri tukijua tofauti iliyopo baina ya kuwa peke yako na upweke.  Hivi ni vitu tofauti: kuwa peke yako inamaanisha kukosa mawasiliano au ukaribu na watu wengine, unakuwa kama uliyetengwa, wakati upweke (loneliness) inahusisha nafsi,  akili na hisia kuwa pweke au kujihisi kutengwa na hii ni ngumu kuishuhulikia.  Ni heri kuwa peke yako (single) kuliko kuwa  kwenye ndoa na bado ukajisikia upweke (lonely).  Wako wengine waliodhani ndoa ni suluhisho la upweke waliokuwa nao na mara walipoolewa au kuoa, mawasiliano baina yao yakayumba na hivyo kukomaza  upweke kwa wote wawili.
  1. Kuolewa au kuoa kwasababu ya shinikizo kutoka kwa wazazi,ndugu au marafiki
Shinikizo hizi zaweza kuwa za kihisia au hata kihalisia.  Kihisia ni pale ndugu au wazazi wanapokushawishi mara kwa mara kuoa sababu umri wako una pita na wako wazazi wengine husema wanataka wajukuu.  Hata kama huhisi  kulazimishwa lakini kwa kule kurudia rudia kwa kukumbushwa kila siku kunaathiri hisia zako na kuweza kukupelekea kuingia katika ndoa isiyopangiliwa.  Shinikizo ya kimwili au kihalisia ni pale wazazi wanopolazimisha watoto wao kuoa au kuolewa na watu fulani kwa sababu tu ni marafiki zao (family friends) au kwa sababu ya kulinda utajiri na matarajio yoyote binafsi.  Ndoa nyingi za aina hii zimekuwa kero na dimbwi la maumivu na machozi, baada ya muda kidogo mna jikuta mali mnazo, wazazi wenu wanapatana,  lakini nyie kama wapenzi ni maadui wakubwa.

  1. Kuamua kuoa au kuolewa ili kupata Uhuru.
Hii hutokea sana kwa wale waliozoea kubanwa sana na wazazi katika kila wafanyacho hususani katika maamuzi.  Wengine huzikimbia familia zao maana hazieleweki, hazina mpangilio na hivyo kutamani kutoka ili wakaanzishe zakwao wenyewe. Kinadada na kinakaka wanachoka kuamuliwa na kuwekewa masharti ya kuvaa, kula, kufanya mambo, kutoka na kurudi kwa muda kwahiyo wanadhani ndoa ndio itawachomoa kifungoni hapo.

MATOKEO YA KUINGIA KATIKA NDOA KWA SABABU MBOVU
Lengo la kuingia kwenye ndoa, liwe zuri au liwe baya ndilo litakalotegemeza aina ya maisha yenu katika ndoa hiyo kuwa ya furaha au ya machungu.  Baada tu ya kuoana na huyo mtu wako kwa sababu zisizo za msingi, siku, miezi au miaka siyo mingi utaanza kuchoka na kutamani kutoka nje ya hiyo ndoa kwamaana baina yenu hakuna muunganiko wa kindani ya ndoa ya jinsi hii.  Na mara nyingi hali hii hupelekea msongo wa mawazo, mfadhaiko na kukosa furaha ndani ya ndoa.  Na matokeo ya hali hii kumfanya mwanandoa mmoja au wote wawili kuanza kutafuta kutoshelezwa na kuliwazwa nje ya ndoa na hapa vinazaliwa vitu kama uzinzi, kutengana na talaka.

Kwanini Ndoa nyingi hushindwa:
Kwa sababu ya kukosa maarifa. Wanandoa wengi hawajui nini wafanye, nini  waelewe ili kufanya ndoa yao zifanikiwe.  Thamani ya ndoa na jinsi ndoa  inavyochukuliwa sikuhizi ni tofauti sana na nyakati za wazazi wetu, na hii imewafanya wengine kujikuta wako wenye ndoa kwasababu mbovu na hivyo ndoa nyingi kuvunjika au kuyumba baada ya muda mfupi tu. Vitu kama kudhamiria, heshima na uaminifu sio vya maana tena siku hizi, sababu watu wanaogopa kuonekana wazamani na washamba. 

Mtazamo wa ulimengu juu ya ndoa umeharibiwa na magazeti, luninga na vitabu mbali mbali.  Siku hizi kuishi bila ndoa ni kitu cha kawaida, kuwa na mpenzi nje ya ndoa sio kitu cha kutisha tena,  mapenzi nje ya ndoa sio ya kushangaza hata kidogo.  Kinyume chake ukionekana kuyashangaa haya, jamii itakushangaa wewe kwa jinsi ulivyo nyuma ya wakati.  Mambo yamebadilika sana, zamani binti akikutwa bikira wakati anaolewa ilikuwa sifa kwake na familia nzima, siku hizi binti akikutwa bikira atachekwa, na watu kumshangaa wakihisi ana matatizo fulani. Hali kadhalika kwa kijana wa kiume aliyejitunza. Kwa bahati mbaya sana  tunaishi katika jamii ya ajabu isiyoamini katika kujitoa kwa kweli na kudhamiria katika ndoa. Jamii isiyoamini katika uaminifu, na ndiyo maana magomvi mengi hutokea pale simu ya mmoja inapoguswa.  Kuwindana na kuchunguzana kumekuwa kawaida, maadili sio jambo la kuzingatiwa tena.  Wanandoa wengi ni wale wenye majeraha ya moyoni na walio umizwa, kwa hiyo hutoka nje ya ndoa zao wakitafutatafuta mwingine aliyeumizwa kama wao ili  waliwazane.

Kwa haraka tuangalie sababu za msingi zinazoweza kukufanya uingie katika ndoa na usijute.
-          Ndoa ni mpango wa Mungu kwa mwanamke na mwanaume kuwa pamoja
-          Ni nafasi ya wawili hawa kuonyeshana mapenzi  yao
-          Ni nafasi ya kutimiziana mahitaji ya mwili kupitia tendo la ndoa kwa muda sahihi, na kwa mtu sahihi, maadili yakizigatiwa.
-          Hamu na kiu ya kutengeneza famila yenu.
-          Kutimiza kiu ya kuwa pamoja kwa umoja (companionship)
-          Nia au kusudi la kushiriki vyote kwa pamoja . Kufanya kutenda kwa pamoja ili kutimiza mahitaji yetu wote.
       -    Nafasi ya kutumia kwa manufaa kila uwezo na vipawa mlivyokuwa    
     navyo.
-          Kuchangiana katika makuzi yenu ya ujumla, makuzi ya kimwili, kiriho, kihisia n.k
 
Na: Chris Mauki
Counselor and Social Psychologist
University of Dar es Salaam
0777 407182, chriss@udsm.ac.tz

Wednesday, October 12, 2011

CAMPUS NIGTHT LAUNCHING PREPARATIONS

Watu mbali mbali wakifanya Registration kwa ajili ya Campus Night 2011. It will be 11.11.11 pale Leaders clubs


Hii ni moja ya Maandalizi ya Campus Night Launching, Pale VCC tarehe 16.10.2011.

Hii itakua ya Aina yake. Njoo Jumapili ya tarehe 16.10.2011 pale VCC upate kujua undani wa Campus night

Friday, September 9, 2011

The bridge Photos

ADD
 Very Hot Praise And Worship
Roho Mtakatisfu anatembea isivyokawaida
The Bridge Felowship

Various Life Education and Biblical Education

Worship

THE BRIDGE MEMBERS WORSHIPING GOD

We worship You our Lord

 Feel free to Worship God


 Deep Worship
 Praise God with Joy

 members
 tHE bRIDGE mEMBERS wORSHIPING GOD

Friendship Love and Affection

 Jamani Shosti, Nilikumissssss hadi basi.......
AH! Mtumishi Tonny Nimefurahi kukuona mtumishi

THE BRIDGE......

AH mtumishi hatujaonana mda mrefu.....

WE BRING  PEOPLE TO JESUSSEE THE BRIDGE MISSION TO LUTINDI TANGA
 











WE REACH SOCIETY
THE BRIDGE MISSION -  LUTINDI - TANGA



GAMES AND MATCH
Chicken Chasing Game: Chairman kashinda Kuku

The Bridge Football Team

 Football Prayers: Unazion njemba Hizi? Noomaa

Assistant Pastor Vedastus Kapongo, 4th from Left, during the match THE BRIDGE YOUTH Vs RIVERS OF JOY PRAISE TEAM
 THE BRIDGE VOLLEYBALL CAPTAIN receiving waning Cup
THE BRIDGE FOOTBALL CUP

GUNNERS

Thursday, September 8, 2011

VICTORIA CHRISTIAN CENTRE: REV ADAM HAJI MOHAMED Born Again Muslim

SEMINAR  SEMINAR SEMINAR
Rev. Dr. Huruma Nkone invites all people to an Exceptional Seminar
"Born again Muslim using bible and koran in his Sermons"

SPEAKER : REV ADAM HAJI MOHAMED 
The anointed man of God from Somaria. The islamic country, a man of God with very sensitive and touching Testimonies.
Date: 8 - 11 September 2011
i.e. Thursday to Sunday
Place: Victoria Christian Centre (At victoria Petrol Station) Mikocheni.


Time table:
Thursday: 08th September 2011-1630 - 1830 hrs E.A time
Friday: 09th September 2011- 1630 - 1830 hrs E.A time
Saturday: 10th september 2011 1530 - 1900 hrs E.A time
SUNDAY:Two Services only
1st Service: English - From 0730 - 1000 hrs
2nd Service: Swahili- From 1015 - 1300 hrs


DO NOT PLAN TO MISS AND GOD BLESS YOU:

Monday, September 5, 2011

How to live good life

Randy Pausch:
This is amazing, he died of pancreatic cancer in 2008, but wrote a book
‘The last lecture” 
 before then, one of the bestsellers in 2007 - New York. What a legacy to leave behind…

In a letter to his wife  and his children,  he wrote this beautiful "Guide to a better life" for them to follow.


POINTS ON HOW TO IMPROVE YOUR LIFE

Personality:
1. Don't compare your life to others'. You have no idea what their journey is all about.
2. Don't have negative thoughts of things you cannot control. Instead invest your energy in the positive present moment
3. Don't overdo; keep your limits
4. Don't take yourself so seriously; no one else does
5. Don't waste your precious energy on gossip
6. Dream more while you are awake
7. Envy is a waste of time. You already have all you need..
8. Forget issues of the past. Don't remind your partner of his/her mistakes of the past. That will ruin your present happiness.
9. Life is too short to waste time hating anyone. Don't hate others.
10. Make peace with your past so it won't spoil the present
11. No one is in charge of your happiness except you
12. Realize that life is a school and you are here to learn.
Problems are simply part of the curriculum that appear and fade away like algebra class but the lessons you learn will last a lifetime.
13. Smile and laugh more
14. You don't have to win every argument. Agree to disagree.


Community:
15. Call your family often
16. Each day give something good to others
17. Forgive everyone for everything
18. Spend time with people over the age of 70 & under the age of 6
19. Try to make at least three people smile each day
20. What other people think of you is none of your business
21. Your job will not take care of you when you are sick. Your family and friends will. Stay in touch.


Life:
22. Put GOD first in anything and everything that you think, say and do.
23. GOD heals everything
24. Do the right things
25. However good or bad a situation is, it will change
26. No matter how you feel, get up, dress up and show up
27. The best is yet to come
28. Get rid of anything that isn't useful, beautiful or joyful
29. When you awake alive in the morning, thank GOD for it
30. If you know GOD you will always be happy. So, be happy.


Sunday, September 4, 2011

SIRI YA TABASAMU
*smile*
Unajua Siri iliyoko katika kutabasamu?

IN SMILE THERE IS LOVE
NDANI YA UPENDO LIMO TABASAMU 

Vipi wewe na umpendaye?

*  Kumjua mtu anayekupenda huburudika kukuangalia usoni kwako mda mrefu.

*  Ukiangaliwa tu, TABASAMU

1. Tabasamu hutufanya tuvutie

Smile makes us cerebrate


2. Kiafya Tabasamu huongeza mfumo wa kinga
Hufanya kinga kufanyakazi kwa spidi maana mwili umejiachia

3. Tabasamu huambukiza furaha kwa watu wengine.
TABASAMU KATIKA PENDO
4.Tabasamu hudumisha upendo na mapenzi.



5.Tabasamu hupunguza Mishtuko ya mwili-Stress 
Stress hutoweka pale tunapotabasamu na kuufanya mweli ujiachie huru 


6 . Tabasamu hupunguza Shinikizo la damu (Blood Pressure)
7. Tabasamu huachilia Endorphins (kituliza Maumivu cha asili) na Serotonin
SMILE HADI BASI
8. Tabasamu hunyanyua uso na kufanya UONEKANE BADO MDOGO. Maana yake ukinuna sura inakuwa kama m-bibi/m-babu 
KAMUA TABASAMU
SMILE FOR FUTURE
9. Tabasamu hufanya mtu awe na mtazamo chanya (positive mind)